EPHRAIM SEKELETI: Muimbaji machachali nchini Zambia



EphraimSekeleeti Mutalange ni muimbaji wa nyimbo za injili nchini Zambia, ambae alianza kuimba akiwa na umri mdogo akiwa kanisani na kupata uzoefu wa kuimba pamoja na kupiga kinanda.
Ephraimu Sekeleti  akiwa anaimba jukwaani


Kadri siku zilivyozidi kwenda akajiunga na kikundi kilichojulikana kama Virtue for Christ ambapo  akiwa katika kikundi hicho  aliimba kwa kipindi wa miaka miwili. Mnamo mwaka 2002 alipata kiasi kidogo cha pesa na kwenda  nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya kurekodi lbamu yake ya kwanza.

Licha ya kuchukua uamuzi huo wa kwenda kurekodi, lakini mambo yalikuwa tofauti na alivyo tarajia, kwani  alifanikiwa kurekodi nyimbo mbili pekee. Akiwa anajaribu kuzoea mazingira alijiunga na kikundi cha maigizo mjini Pritoria na kupata nafa ya kuimba mbele ya raisi.

Wakati nafasi nyingi zilivyozidi kujitokeza zililimfanya awaze kuachana na muziki wa injili na kuimba nyimbo za kidunia, lakini alijitahidi kuwa mwaminifu na kuendelea na muziki wa injili.

Kadri sikuku zilivyozidi kwenda, hatimaye mlango ukafunguka na akapata nafasi ya kurekodi albamu yake ya kwanza iliyo julikana kama Temba Baby, pamoja na kupata mafanikio katika albamu hii ambayo yalimpelekea ajisikie kurudi nyumbani kwao nchini Zambia na kuwekeza pesa alizopata kwa ajili ya albamu ya pili na kufanikiwa kuitoa ambayo ilikuwa inajilikana kama Limo Ndanaka.

Albamu hii ya pili ilifanya vizuri kwa wakristo na kushika nafasi ya juu katika muziki wa injili. Pia Ephraim alipata  nafasi kutembelea nchi mbalimbali kwa ajili ya uimbaji  nje ya Zambia , kama vile Namibia, Afrika ya Kusini, Tanzania, Zimbabwe na Autralia. Kijana huyu mdogo ni mfano wa  waimbaji wanaoiwakilisha nchi ya Zambia kwa kile anachokifanya.


Pamoja na kufanya muziki nchini Zambia, lakini pia kuna albamu yake aliyoimba kwa lugha ya kiswahili ambayo ilitafsiriwa kutoka lugha ya kizamzia, moja ya nyimbo hizo ni kama vile  Uniongoze na uruma zako, Moto unawaka, Mungu usiyelala nanyingine ambazo aliirekodia nchini Tanzania.
Ephraim sekeleti amezaliwa septemba 26, 1983 kalulushi nchini Zambia.Pia albamu alizonazo mpaka sasa ni pamoja na Temba Baby, Limo Ndanaka, Lesa Tekeleshi, Lekeni Iloke na nyinginezo.

Comments

Popular posts from this blog

Ambwene Mwasongwe: Msanii anaekonga mioyo ya watu

Historia ya muziki wa injili

REBECCA MALOPE: Malkia wa muziki wa injili Afrika ya Kusini