Pata kumfahamu muimbaji mahiri Solly Mahlangu.
Muimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili, ambae pia ni Mchungaji Solly
Mahlangu, ni moja kati ya wimbaji maarufu kutoka nchini Afrika ya kusini,
barani Afrika. Ni msanii ambae amekuwa akiimba nyimbo zake moja kwa moja akiwa
jukwaani kwa kutumia na vyombo mbalimbali vya kisasa vya muziki, tofauti na
tulivyo zoea kuona wasanii wengine
wakirekodi kwanza nyimbo zao studio, na baadae kutumia kanda wanapokuwa wanaimba
katika majukwaa japo kwa sasa baadhi yao
wameanza kufanya kama Mahalangu.
Mahalangu amekuwa akifanya
muziki ambao unawavutia watu wengi sana ulimwenguni, kutokana na uimbaji wake
wa kipekee pamoja na ubunifu alionao akiwa anaibma jukwaani
Mahalangu ni msanii ambae amezaliwa mjini Johannesburg nchini Afrika ya kusini 1971, amelelewa na mamayake,
pia aliokoka akiwa na umri dogogo .
Ameanza utumishi wa uimbaji wa nyimbo za injili akiwa na miaka 10 ambapo
maishayake yote tangu utoto amekua akiishi,
mjini Johanessesburg.
Akiwa umri wa
miaka 18 alichukua uamuzi wa
kufunga ndoa na mke wake mpendwa Khosi Mahalangu, katika ndoa yao, pia
wamejaliwa watoto watatu wa kike ambao ni Thando, Amani na Asante.
Baada ya kutumika kwa muda wa miaka 20 katika huduma hiyo kama kiongozi wa kuabudu na mkurugenzi wa
muziki, baadaye akawa mkurugenzi wa muziki kitaifa katika Kanisa la Victory
Fellowship chini ya Dk. M.A. Maphalala .Akiwa kwenye
huduma ya uimbaji, aliweza kusafiri nchi mbalimbali zilizopo barani Afrika akiwa pia kama kiongozi wa mafunzo ya
masuala ya kiroho.
.
Pia
mchungaji Mahlangu katika uimbaji wake
ni mzoefu wa kurekodi muziki tangu 1991, akiwa na jumla ya albamu nne ambazo ni
PRAISE HIM IN AFRICA 1970, MWAMBAMWAMBA, NGISONDELA KUWE 2014NA OBRIGADO 2010.
Hata hivyo amekuwa kiongozi wa kanisa ambalo alianzisha linaloitwa Word Praise Christian Center
International lililopo eneo la Tembiza mjini Johanesburg.
Kanisa hilo likiwa Chini ya
Mchungaji mahlangu akisaidiana na mkewe
katika uangalizi, kanisa hilo likazidi kukua na kupata umaarufu mkubwa.
Miongoni mwa albamu zilizo bamba zaidi kitaifa na kimataifa ambazo ameimba moja
kwa moja ‘live’ katika matamasha ya kimataifa kwa njia ya DVD na CD ni Obrigado
na Mwamba Mwamba.
Pia Mchungaji mahlangu amekuwa akifanya huduma ya
uimbaji sambamba na kuendesha kanisa
jambo ambalo katika mazingira ya kawaida ni watu wachache sana wanaweza kufanya
hivyo hiki ni kitu cha kuvutia zaidi
Mwaka 2002 aliibuka mshindi wa tuzo tatu za SABC Gospel Crown
Awards tukio ambalo liliwashangaza wengi. Vilevile kutokana na kudhiirisha
ubora wa nyimbo anazoimba, akaingia tena kwenye tuzo ya 18 ya MTN South African
Music Awards.Mahlangu pia amewahi kuingia katika shindano la kuwania tuzo ya albamu bora ya Best Traditional Faith Music na Best live DVD akishindana na wakali wenzake kama Concord Nkabinde na Simphiwe Dana.


Iko poa my dada
ReplyDelete