Posts

Showing posts from 2015

REBECCA MALOPE: Malkia wa muziki wa injili Afrika ya Kusini

Image
Rebecca Malope amezaliwa mwaka 1968 karibu na Nelspruit mji mkuu wa Mpumalanga, Siku za nyuma alikuwa hawezi kutembea umbali mrefu hivyo alishindwa kuendelea kusoma, kiufupi tu ni kwamba alipokuwa motto mdogo alikuwa akitumia baiskeli za walemavu kutembelea kutokana na kuumwa sana na kwa muda mrefu ambapo iliwapelekea hata madaktari kuamini kwamba hataweza kutembea tena. Malkia wa nyimbo za injili Afrika ya Kusini Rebecca Malope akiwa ameshika tuzo. Familia yake ilikuwa maskini sana, ambapo mnamo mwaka 1986 Rebeka pamoja na dada yake Cynthia walitembea umbali wa kilomita 400 kutoka nyumbani kwao kwenda   Johannesburg mjini Evaton kutafuta kazi. Mnamo mwaka 1986 Rebecca aliingia kikundi cha kusaka vipaji kilichojulikana kama ‘Shell Road Fame’ lakini hakufanikiwa.   Hakujali hilo akaingia tena mwaka uliofata na hatimae akashinda kuwa mwimbaji bora katika aina ya usololisti pamoja na Shine On . Tuzo aliyoipata baada ya kuwa mshindi iliwakilisha katika soko la muzi...

ROSE MUHANDO: Malkia wa muziki wa injili nchi Tanzania

Image
Rose mhando ni muimbaji   maarufu wa nyimbo za   injili nchini Tanzania na afrika ya mashariki kwa ujumla ambaye alianza kutambwa mwaka 2004 na albamu ya Uwe Macho ambayo ilipendwa na watu wengisana. Awali muimbaji huyu kabla ya kuwa mkristo, alikuwa muumini wa dini ya kiislamu, baadaye alipokuwa na umri wa miaka tisa anasema akiwa amelala alipata maono ya Yesu Kristo. Pia anasema aliteseka kwa muda wa miaka mitatu na kuamua kubadilisha dini kwa kupokea wokovu na kuwa mkristo, ambapo baadaye alianza kuimba muziki wa injili kama mwalimu wa kwaya inayojulikana kama kwaya ya Mtakatifu Maria katika kanisa la Anglikana linalofahamika kama Chimuli lilipo mkoani Dodoma. Tangu aanze kuimba muziki wa injili amefani kiwa kutunukiwa tuzo tatu ambapo tuzo ya kwanza alitunukiwa tuzo ya muimbaji bora wa kike na nyimbo za dini 2005 tuzo ya Tanzania Music Award wimbo ukiwa “Mteule uwe macho”, 2009 alipata tuzo ya Tanzania Gospel Singer Awards ya mwimbaji bora nchini Tanza...

EPHRAIM SEKELETI: Muimbaji machachali nchini Zambia

Image
EphraimSekeleeti Mutalange ni muimbaji wa nyimbo za injili nchini Zambia, ambae alianza kuimba akiwa na umri mdogo akiwa kanisani na kupata uzoefu wa kuimba pamoja na kupiga kinanda. Ephraimu Sekeleti  akiwa anaimba jukwaani Kadri siku zilivyozidi kwenda akajiunga na kikundi kilichojulikana kama Virtue for Christ ambapo   akiwa katika kikundi hicho   aliimba kwa kipindi wa miaka miwili. Mnamo mwaka 2002 alipata kiasi kidogo cha pesa na kwenda   nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya kurekodi lbamu yake ya kwanza. Licha ya kuchukua uamuzi huo wa kwenda kurekodi, lakini mambo yalikuwa tofauti na alivyo tarajia, kwani   alifanikiwa kurekodi nyimbo mbili pekee. Akiwa anajaribu kuzoea mazingira alijiunga na kikundi cha maigizo mjini Pritoria na kupata nafa ya kuimba mbele ya raisi. Wakati nafasi nyingi zilivyozidi kujitokeza zililimfanya awaze kuachana na muziki wa injili na kuimba nyimbo za kidunia, lakini alijitahidi kuwa mwaminifu na kuende...

Ambwene Mwasongwe: Msanii anaekonga mioyo ya watu

Image
Ambwene Mwasongwe ni msanii ambae nyimbo zake zimebeba ujumbe murua,   ambao unawavutia watu wa aina mbalimbali walio wakristo na hatata watu wa dini zingine   kusikiliza. Mwasongwe amekuwa na uimbaji wa tofauti na wasanii wengine Afrika ya mashariki na barani Afrika , hasa katika utunzi wa nyimbo zake ambazo zinakuwa zimebeba ujumbe mzito ambao mtu yeyote akisikiliza zinamfanya atafakari zaidi. Ambwene Mwasonwe akiwa anaimba. Moja kati ya nyimbo zake ambazo watu wengi wamekuwa wakipenda kusikiliza ni MAJARIBU NI MTAJI, MISULI YA IMANI na UPENDO WAKWELI hizi ni baadhi ya nyimbo za Mwasongwe   ambazo   zinasikilizwa kwa kiasi kikubwa. Msanii huyu amezaliwa mwaka 1985, ambapo alianza kuimba nyimbo za injili akiwa na umri wa miaka 16 na kutoa albamu yake ya kwanza inyoitwa Majaribu ni mtaji , akiwa na miaka 19, ikiwa mpaka sasa ametoa albamu tatu yapili ikiitwa Heshima ya mrefu ni mfupi maarufu kama mzee wa siku, na ya tatu ni Misuli ya imani. ...

Pata kumfahamu muimbaji mahiri Solly Mahlangu.

Image
Muimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili, ambae pia ni Mchungaji Solly Mahlangu, ni moja kati ya wimbaji maarufu kutoka nchini Afrika ya kusini, barani Afrika. Ni msanii ambae amekuwa akiimba nyimbo zake moja kwa moja akiwa jukwaani kwa kutumia na vyombo mbalimbali vya kisasa vya muziki, tofauti na tulivyo zoea kuona   wasanii wengine wakirekodi kwanza nyimbo zao studio, na baadae kutumia kanda wanapokuwa wanaimba katika majukwaa   japo kwa sasa baadhi yao wameanza kufanya kama Mahalangu.   Mwimbaji ambae pia ni Mchungaji Solly Mahlangu akiwa jukwaani .      Mahalangu amekuwa akifanya muziki ambao unawavutia watu wengi sana ulimwenguni, kutokana na uimbaji wake wa kipekee pamoja na ubunifu alionao akiwa   anaibma jukwaani Mahalangu   ni msanii ambae   amezaliwa mjini Johannesburg nchini   Afrika ya kusini 1971, amelelewa na mamayake, pia aliokoka   akiwa na umri dogogo . Ameanza utumishi wa uimbaji wa nyimb...

Historia ya muziki wa injili

Image
Je umewahi kusikia wimbo ambao umekutoa sehemu ulipo na unataka kuwaeleza rafiki zako kuhusiana na hicho ulichokisikiliza? Vizuri hii ni aina ya hisia uliyowahi kuiskia kutoka kwenye nyimbo za injili. Kwa uhalisia, neno Injili inamaanisha habari njema. Muziki wa injili ni moja ya chombo bora  cha usafiri ambacho uaminika na wakristo katika kueneza injili kwa wasikilizaji ulimwenguni kote.  Muziki huu  ulichipuka katika tamaduni za kitajiri katika  makanisa ya kiafrika na kimarekani kuanzia miaka ya 1800, Makanisa hayo yalioko huko   umoja wa Marekani kusini ya alianza kukusanyika katika mitindo  mbalimbali ya muziki kwenye  ibada  za kuabudu  pamoja na kusifu katika roho pamoja na nyimbo za zaburi. Aina ya muziki uliokuwa ukiimbwa awali kanisani ulikuwa ukihusisha kupiga makofi na kucheza stepu. Moyo wa utamaduni  wa muziki wa injili ulikuwa ukitumia kwaya. Kwaya za kanisa zilikuwa zikiundwa na kundi la waimbaji a...