ROSE MUHANDO: Malkia wa muziki wa injili nchi Tanzania



Rose mhando ni muimbaji  maarufu wa nyimbo za  injili nchini Tanzania na afrika ya mashariki kwa ujumla ambaye alianza kutambwa mwaka 2004 na albamu ya Uwe Macho ambayo ilipendwa na watu wengisana.



Awali muimbaji huyu kabla ya kuwa mkristo, alikuwa muumini wa dini ya kiislamu, baadaye alipokuwa na umri wa miaka tisa anasema akiwa amelala alipata maono ya Yesu Kristo.

Pia anasema aliteseka kwa muda wa miaka mitatu na kuamua kubadilisha dini kwa kupokea wokovu na kuwa mkristo, ambapo baadaye alianza kuimba muziki wa injili kama mwalimu wa kwaya inayojulikana kama kwaya ya Mtakatifu Maria katika kanisa la Anglikana linalofahamika kama Chimuli lilipo mkoani Dodoma.

Tangu aanze kuimba muziki wa injili amefani kiwa kutunukiwa tuzo tatu ambapo tuzo ya kwanza alitunukiwa tuzo ya muimbaji bora wa kike na nyimbo za dini 2005 tuzo ya Tanzania Music Award wimbo ukiwa “Mteule uwe macho”, 2009 alipata tuzo ya Tanzania Gospel Singer Awards ya mwimbaji bora nchini Tanzania ambapo alizawadiwa fedha za kitanzania sh. 200,000, vilevile 20o8 alipata tuzo ya Kenya Groove Award ya muimbaji bora wa kike barani Afrika.

Rose Muhando akiwa ameshika tuzo



Rose Muhando amezaliwa mwaka 1976 katika kijiji cha Dumila, Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro nchini Tanzania na ni mama wa watoto watatu, ambapo mpaka sasa amefanikiwa kutoa kadhaa kamavile Uwe Macho 2004,  kwaya ya Kitimtim jina la albamu Uinuliwe Baba2005, Jipange Sawasawa 2008, Utamu wa Yesu, na Pindo la yesu, kwa sasa anatamba na wimbo wa Facebook.

Comments

Popular posts from this blog

Ambwene Mwasongwe: Msanii anaekonga mioyo ya watu

Historia ya muziki wa injili

REBECCA MALOPE: Malkia wa muziki wa injili Afrika ya Kusini